Matajiri wa Jangwan Klabu ya Yanga Sc inadaiwa kuwa imevunja ndoa yake na mchezaji wake Juma Makapu ambaye ameitumikia klabu hiyo kwa muda mrefu.

Makapu amekuwa na kikosi cha Yanga Sc kwa Zaidi ya Misimu Mitano lakini ameshindwa kushawishi walimu kutumika katika kikosi cha kwanza.

Makapu mwenye uwezo wa kucheza kwa ufasaha nafasi ya kiungo mkabaji, beki ya kati na kulia,anahusishwa na kusajiliwa na Timu ya Mtibwa Sukari yenye Makao yake Makuu Turiani Mkoani Morogoro

Juma Makapu alijiunga na Yanga kwa Mra ya Kwanza mwaka 2014 akitokea katika Klabu ya Shangani Visiwani Zanzibar wakati huo yanga ikinolewa na Kocha Mwenye asili ya Kibrazil Marcio Maximo.