Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman ameitaja Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia wazee na watoto katika orodha ya taasisi zisizozingatia nidhamu katika matumizi ya fedha za Serikali.
Amesema hayo leo katika ziara yake kwenye Hospital
ya Rufaa ya Mnazi Moja ambapo amemuagiza Waziri wa wizara hiyo, Nassor Mazrui kuhakikisha
dawa na Vifaa tiba vinavyonunuliwa viwe vinaendana na Thamani halisi ya Fedha
inayotumika.
Mhe. Hemed amesema Serikali ya awamu ya nane
inayoongozwa na Rais Dkt. Mwinyi imedhamiria kudhibiti matumizi ya Fedha za Serikali
na itakapobidi haitasita kubadilisha baadhi ya sheria ili kufanikisha lengo
hilo.
Pamoja na hayo ameeleza kusikitishwa kwa kusuasua
kwa huduma ya upatikanaji wa mashuka kwa wakati kulikosababishwa na kuharibika
kwa kifaa cha mashine ya kufulia, kifaa ambacho harama yake haizidi sh. Laki
Nne.
Nae, Mkurugenzi Mtendaji wa Hopital ya Rufaa ya
Mnazi Mmoja Dkt. Msafiri Marijani amemueleza Mhe. Hemed kuwa wanakabiliwa na
changamoto tofauti ikiwemo upungufu wa wataalamu wa kada mbali mbali, uhaba wa
idadi ya Vyumba vya kuendesha matibabu ya upasuaji pamoja na upungufu wa
Vitendanishi kwa ajili ya kufanya vipimo katika maabara.





0 Maoni