Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo ambae pia ni Makamo wa kwanza wa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Othman Msoud Othman amesema ataiendeleza kwa Juhudi na hekma kubwa kazi iliyofanywa na Mtangulizi wake marehemu Maalim Seif Sharif Hamad katika kuhakikisha Zanzibar inapata maendeleo.

Mhe. Othman ameyasema hayo Kisiwani Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati akizungumza na wananchama wa Chama hicho katika ziara rasmi ya  kujitambulisha katika jimbo hilo .

Amesema ni vema wananchi wakaendelea kutekeleza jambo muhimu la kujenga umoja kama lilivyo asisiwa na mtangulizi wake  ili kuungana na viongozi wa kitaifa katika juhudi kubwa wanazozifanya za kuunganisha watu na kupigania  haki na maendeleo.

‘‘ wananchi  wanapaswa Msivunjike moyo kwakua viongozi wenu tunajitahidi kupigania uwajibikaji na uwadilifu katika Serikali  kwa kuwa ndio njia muhimu zaidi  ya kuleta maendeleo ya Zanzibar’’

Katika hatua  nyengine Mhe Othman amesema  Chama hicho kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa kumetokana na hekima na maauzi ya chama hicho na kwamba kazi ya kusimamia suala hilo alilokabidhiwa ni jambo kubwa na ataifanya kwa juhudi na hekima kubwa ili wananchi wa Zanzibar wamapete maendeleo kama ilivyokusudiwa.

 Mapema Mhe. Othman alikutana na wazee wa Chama cha ACT Jimbo la Tumbatu kwa nia ya kujitambulisha kwa wazee hao kutokana na kukabidhiwa jukumu kubwa la uongozi wa Zanzibar.

Katika ziara hiyo Mhe. Othman aliambatana na Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mhe. Juma Duni Haji,Kaimu

 Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar Salim Biman, Naibu Katibu wa Idara ya Organizetion, Omar Ali Shehe pamoja na viongozi wengine mbali mbali.