Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akikagua maeneo mbali mbali katika Hospital ya wagonjwa wa akili ya Kidongochekundu kufuatia ziara ya kushtukiza alioifanya leo kwa ajili ya kujionea huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Na mwandishi wetu

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka uongozi wa Wizara ya Afya kutatua changamoto ya kukosekana kwa Vifa tiba katika Hospital na vituo vya Afya Nchini Ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Hemed ameeleza hayo katika ziara yake ya kushtukiza Hospitali ya Mwembeladu na Hospital ya Wagonjwa wa akili Kidongo Chekundo kwa lengo la kujionea huduma zinavyotolewa kwa wananchi wanaofika katika Hospitali hizo.

Amesema viongozi wenye dhamana ya kusimamia vituo vya Afya wana jukumu la kuhakikisha vifaa tiba vinavyohitajika vinapatikana kwa wakati sambamba na kufanya ukarabati wa maeneo mbali mbali ili kuweka mazingira bora kwa wafanya kazi wanaotoa huduma kwa wananchi.

Wakati ametembelea Hospital ya Mwembeladu Makamu wa Pili wa Rais amesema maeneo ya kufanyia kazi kwa madktari katika hospital hiyo sio ya kuridhisha, hivyo amemuagiza Mkurgenzi Mtendaji wa Hospital ya Mnazi Moja Dk. Msafiri Marijani kuchukua hatua za haraka kwa kufanya ukarabati wa kawaida katika baadhi ya maeneo.

Akikagua sehemu ya kuhifadhia dawa na vifaa tiba Mhe. Hemed alimuelekeza Dk. Marijani kuhakikisha vifaa tiba ikiwemo mikoba ya kujifungulia pamoja na dawa muhimu zinazopatikana katika bohari kuu ya Serikali zinapatikana kwa wakati katika Hospital hizo.

                                                  

Mmoja ya wananchi waliofika katika Hospital ya Mwembeladu akimueleza Makamu wa Pili wa Rais changamoto wanazokabiliana nazo ikiwemo kukosekana kwa kipimo cha damu katika Hospital hiyo.

Mhe. Hemed akizungunza na wananchi waliofika kupata huduma katika Hospital ya Mwembeladu huku akiwaelezea adhama ya serikali ya awamu wa nane katika kutatua changamoto za sekta ya Afya kwa ajili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi wake.