Mkuu wa Kikosi Maalum Cha Kuzuia Magendo (KMKM) COMMODORE Azana Hassan Msingiri akimkaribisha Mtendaji mkuu Ofisi ya Rais Ikulu (Mlikulu) Mahmoud Othman mara alipofika Ofisini hapo kwaajili ya kuopokea samaki waliovuliwa na kikosi hicho kwaniaba ya Rais wa Zanzibar Huko Ofisi za (KMKM) Kibweni Zanzibar.
Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) kimeeleza
kuwa kinathamini na kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
katika kuinua uchumi kupitia Bahari kuu.
Mkuu wa Kikosi cha KMKM Zanzibar, Commodore Azana
Msingiri amesema kikosi hicho kimejipanga katika kuimarisha upatikanaji wa
samaki wakubwa kwa kutumia vifaa na uvuvi wa kisasa ili kufikia azma ya
serikali ya Uchumi wa Buluu.
Amesema katika kipindi cha majaribio Kikosi hicho
kimevua samaki wakubwa katika bahari ya Zanzibar ikiwemo aina ya jodari na
papa.
Commodore Msingiri ameeleza hayo katika hafla ya
kukabidhi samaki waliovuliwa na kikosi cha (KMKM) Makao Makuu ya Kikosi hicho
Kibweni Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha ameeleza kuwa kikosi chake kimepanga kupeleka
watendaji wa kikosi hicho pamoja na vifaa Kisiwani Pemba kwa ajili ya doria ya
kudhibiti magendo ya karafuu katika kipindi hichi cha uchumaji wa zao hilo
unaoendelea.
Nae Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais Ikulu (Mlikulu)
Mahmoud Othman ameikipongeza kikosi cha KMKM na kukitaka kuimarisha doria ili
kuepukana na magendo.
Kwa upande wake Kamanda Hussein Ali Makame Mkuu wa
doria KMKM amesema kikosi kinafanyakazi kwa vitendo katika kuimarisha uchumi wa
buluu pamoja kuzuia magendo nchini.




0 Maoni