Mahakama ya Kisutu imeahirisha Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na Maendeleo Chadema Freman Mbowe na wenzake watatu hadi Agosti 13, 2021.

 Kesi hyo imeghairishwa baada ya upande wa Serikali kudai taratibu za kuifungua kesi hiyo katika Mahakama yenye mamlaka ya kuisikiliza kutokamlika.

Washtakiwa hao wamefikishwa Mahakamani hapo  leo Ijumaa, Agosti 6, 2021  asubuhi wakiwa kwenye basi dogo la Magereza likisindikizwa na magari mawili ya wazi yenye askari magereza.

Baada ya kuwasili washtakiwa wote walishuka na kuelekea kwenye mahabusu ya Mahakama. Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Halfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Lingwenya.