Mkuu wa Wilaya ya Magharibi A, Suzan Kunambi amewataka Madiwani wa Manispaa hiyo, kusimamia vyema vyanzo vya mapato ili kufikia malengo ya Serikali katika kukuza uchumi na kutoa huduma bora kwa Wananchi.
Akifungua kikao cha Madiwani wa Manispaa
ya Magharib A cha utekelezaji kwa kipindi cha robo ya nne
April/ June 2020/2021 kwenye ukumbi wa Manispaa
amesema ukusanyaji unaofanywa kwa njia ya kieletroni utaweza kuleta mabadiliko
na kuuzuia mianya ya upotevu wa fedha kupitia vianzio vyake.
Nae kaimu Mkurgenzi wa Manispaa ya
Magharib A, Amour Ali Abdullah akiwasilisha taarifa ya utekelezaji
wa robo ya nne ya kikao cha mabaraza ya Madiwani
amesema kwa kindipi kifupi wameweza kuvuka malengo ya ukusanyaji
wa mapato kupitia mfumo mpya wa ukusanyaji na kufikia asilimia 7 sawa na
Shilingi Milioni Mia mbili themanini na Tatu, Laki Sita
Tisini Nne Elf na Mia nne themanini na
sita (Tz sh.283,694,486) ambavyo vinatokana na vianzio vyake vya
ndani
Akizungumza kwa niaba ya Madiwan wenzake Diwani viti maalum Khaitham Muhdini Khamis amesema wamejiunga kupitia kamati yao ya sheria na utawala kwa kusimamia vyema majukumu yao kwa maslahi ya jamii.





0 Maoni