Na mwandishi wetu
Chuo Kikuu cha St. Augutine cha Tanzania (SAUT)
kinatarajia kuanzisha tawi lake Zanzibar kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu
nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari Mkuu wa chuo hicho tawi la Dar es salam Ananias Aloys
Rutambuka katika Ukumbi wa Wizara ya
Utalii na Mambo ya Kale Kikwajuni, amesema kuanzishwa tawi hilo Zanzibar
itasaidia kuondoa usumbufu wa wanafunzi kufuata elimu ya juu katika maeneo ya mbali
Amesema tayari wameshaanza kufanya taratibu za
kusajili tawi hilo kuwepo Zanzibar kwa kufuata kanuni zilizowekwa ili
kuanczishwa chuo hicho.
Amesema kuwa vyuo vya elimu ya juu ni muhimu kwani
vinasaidia kuleta maendeleo na uwataka vijana wa Zanzibar kujiunga na vyuo vya
Elimuya juu ili kujifunza kitaaluma.
“Katika kupambana na Sayansi na Technolojia
iliyopo lazima watanzania wajiendeleze
zaidi kielimu ili kufikia malengo
waliyojiwekea hivyo ni wajibu wa vijana kujiunga katika vyuo mbalimbali vilivyopo
nchini”, amefahamisha Mkuu huyo.
Mkuu huyo wa Chuo amewasisitiza vijana wanaotaka
kujiendeleza kielimu kuomba mikopo katika Bodi ya Mikopo kwa lengo la
kuwasidia kimasomo zaidi pamoja
na kulipa deni baada ya kumaliza masomo yao ili na wengine wanufaike.
Nae mhitimu wa Chuo cha SAUT Suleiman Abdallah ambae
pia ni mwandishi wa habari amewashauri wanahabari kujiunga na chuo hicho ili
kuendeleza fani zao na kuweza kufanyakazi kiufanisi zaidi.
CAPTION: Mkuu wa chuo kikuu cha St .Augutine cha Tanzania (SAUT)
tawi la Dar es salam Ananias Aloys Rutambuka akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu wanafunzi kujiunga na elimu ya juu nchini katika Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni Mjini
Zanzibar .




0 Maoni