Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imekusanya sh. bilioni 48.4 tangu ilipoanza kukusanya tozo za miamala ya simu mwezi mmoja uliopita.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini
Dar-es-salaam amesema fedha zilizopatikana baada ya ukusanyaji wa tozo tangu
sheria ilipoanza kutumika mwezi mmoja uliopita,
zimetumika kuboresha sekta ya afya,
elimu na miundombinu.
Hata hivyo amewasihi wananchi kuendelea kuvumilia
suala la tozo za miamala wakati Serikali ikipanga kukutana na watoa huduma wa
mitandao ya simu juu ya majadiliano ya kupunguza gharama za tozo kwa pande zote
mbili.
Amesema tozo za miamala ya simu si michango ya
kirafiki ni sheria iliyopitishwa na
Bunge baada ya kujadiliwa kwa kina
akibainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi.
Dkt. Nchemba ameongeza kuwa nchi ndio zinavyojengwa hivyo amewapongeza
watanzania wote ambao wanatoa mawazo mazuri ya kuboresha jambo hilo.




0 Maoni