Aliyewahi
kuwa Waziri wa Fedha wa Tanzania, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo katika
Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam wakati akipatiwa matibabu.
Mtoto
wa Marehemu Mramba, Godfrey Mramba imesema baba yake amekutwa na umauti leo
asubuhi wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Regency.
Hata
hivyo, ameweka wazi kuwa kutokana na janga la Covid-19 ni wanafamilia wachache
wataruhusiwa kufika kutoa pole nyumbani kwa marehemu, Mawenzi Road, Oysterbay
Dar es Salaam.
Marehemu
Mramba aliwahi kuwa Waziri wa Fedha katika utawala wa Rais Jakaya Mrisho
Kikwete ambapo aliiongoza Wizara hiyo mwaka 2001-2005, baadaye Waziri wa
Viwanda, Biashara na Masoko mwaka 2006 hadi 2008.





0 Maoni