Baada ya Pambano la Ngumi kumalizika Jana (Agust 20) kati ya Dulla Mbabe na Twaha Kiduku  kumalizika na hatimae Twaha Kiduku kushinda,   Tambo za ushindi huo zikaamia mitandaoni

Kupitia mtandao wake wa Kijamii Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Hamisi TaleTale 'Babu Tale' amesema yupo tayari kutoa gari aina ya V8 2020 ili Bondia Twaha Kiduku wa Morogoro na Hassan Mwakinyo wa Tanga wapande ulingoni kuzichapa.

Kauli ya Tale inakuja mara baada ya hapo Twaha Kiduku kumchapa Dullah Mbabe kwa pointi na kuondoka na gari aina ya Toyota Crown.

“Wapeni salaam Morogoro ndio mkoa pekee unaobeba magari yenu yote ya Dar. Tanga eeeh kubalini basi tumalize hili jambo, naweka V8 ya mwaka 2020. Oya Mwana FA mjuze mwanao basi. Asante Twaha Kiduku umetuheshimisha wana Morogoro”amesema Babu Tale.

Mbunge wa Muheza Tanga  nae alijibu suala hilo kwa kumtaka  Babu Tale waandae pambano lenye mkanda.