Na Mwandishi wetu
Mkuu wa Mkoawa Kaskazini Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud amewahimiza wakazi wa Nungwi kuendeleza utamaduni wao ili kuwanusuru Vijana kujiingiza katika mambo maovu.
Akifungua mashindano
ya Qur-an ya QAl-madrasatul-Rahma
Qur-nia iliyopo Nungwi ikiwa
ni tathmini ya uhifadhi wa Qur-an
kipindi cha robo Mwaka
katika Madrasa hiyo
Mkuuwa Mkoa Ayoub amesema
kuwalea watoto katika
misingi ya Dini
ya Kiislamu ni
utamaduni wa Kizanzibar
hivyo ni wajibu
wa jamii kuhakikisha Watoto wao wanakwenda Madrasa.
Amesema utu wa mtu
unatokana na utamaduni hivyo kuwacha utamaduni
wako na kufuata utamaduni wa
kigeni ni kiashiria cha kupoteza
utu .
Akisoma
risala ya Madrasa hiyo
Ostadh Hamadi Shehe
Makame amesema ingawa
wamefanikiwa kuwahifadhisha Qur-an Watoto
zaidi ya mia nne lakini
bado Madrasa inakabiliwa
na upungufu wa Madarasa
, vikalio, vyoo pamoja na
kukabiliwa na mmomonyoko wa maadili
kwa wakazi wa Nungwi jambo ambalo
linarejesha nyuma jitihada za
walimu na wazazi
za kuwalea watoto
katika misingi ya
dini.
Mwalimu
Mkuu wa Madrasa
hiyo Wadi Makame Silima
amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa
msaada wa matofali na
mchanga kwa ajili ya
ujenzi wa madrasa
yao na kuwataka
waislamu wote wa Nungwi
kuwasikiliza viongozi wa
Dini na Serikali
katika mambo ya
kheri wanayo elekeza.





0 Maoni