Mbunge wa Jimbo la Kawe Jijini Dar Es Salam na Askofu wa Kanisa Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema tayari ameshapokea barua ya wito wa kuitwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge Jijini Dodoma.


Jana,katika mitandao mbalimbali  ilisambaa mitandaoni ya barua ya ofisi ya Bunge ikionyesha Gwajima na mbunge wa Ukonga, Jerry Slaa wanatakiwa kwenda mbele ya kamati hiyo Agosti 23 na 24.


“Nimepokea barua ya Spika kwenda kwenye kamati, nitakwenda. Nimesema hapa kwa kuwa aliyenitumia barua ameweka mitandaoni akisema kwanini nimesema hapa na yeye aniambie kwa nini aliweka mitandaoni,” amesema Gwajima leo, Agosti 22, 2021 alipokuwa akizungumza na waumini wake katika kanisa hilo, Dare es Salaam.


Askofu Gwajima amesema atakwenda kwenye kamati hiyo na atasimamia ukweli kama ambavyo imani yake inamtuma.

“Nitakwenda kwenye kamati wategemee ukweli nitasema ukweli kwa kuwa imani ya CCM ni ukweli na nitaongeza mengine ambayo sijawahi kusema. Lazima tusimamie nchi na watoto wa watoto wetu,” amesema askofu Gwajima.

Tukio hilo linajiri baada ya hivi karibuni Spika wa Bunge wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Job Ndugai kuwataka wabunge hao kufika mbele ya kamati ya Maadili ya Bunge kwaajili ya kuhojiwa kuhusiana na mambo ya Covid waliyokuwa wakiyazungumza