Jeshi la Polisi
Mkoani Manyara linamshikilia
Mwanaume Mmoja ajulikanae kwa jina la Harod Hhando Mkazi wa Mtaa wa Silaloda Mji wa Mbulu Mkoani
Manyara, kwa tuhuma za kumuua mtoto wa kaka yake, Emmanuela Hhando (13) na
kumtoa viungo vya mwili.
Taarifa yake aliyoitoa kwa njia ya Simu Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Marrison Mwakyoma
amesema Hhando anahusishwa na mauaji ya mtoto
huyo kwa kumpasua katikati ya miguu na kumtenganisha vipande viwili kisha
kukata sehemu za siri, kumtoa maini na kutaka kuyapika kama mboga kwaajili ya
kula.
Kamanda Mwakyoma amesema tukio hilo lilitokea juzi
August 21,2021 katika kijijinicha Silaloda .
Kamanda Mwakyoma amesema chanzo cha tukio hilo ni imani
za ushirikina baada ya Hhando kuelezwa na anaedaiwa kuwa ni mungu wake amuue
mtoto wa kaka yake na kula maini ili avune mazao mengi.





0 Maoni