Hivi karibuni Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DR Hussein Ally Mwinyi alifanya ziara katika Wilaya zote za Unguja na katika ziara hizo yapo madudu kadhaa aliyoeleza kuyabaini katika kila Halmashauri.

Wakati anafanya majumuisho ya ziara hiyo akiwa ndani ya Mkoa wa Mjini Magharib Raisi alieleza kusikitishwa na kitendo cha Mabaraza ya Mji /Manspaa Kutumia kiwango kikubwa cha pesa walizokusanya kwa wananchi kama sehemu ya Kodi kwa Halmashauri hizo kutumika katika shughuli za kawaida  huku fedha chake pekee ndo hupeleka katika shuhuli za maendeleo kwa Wananchi.

 Jambo hilo lilichangia nalo Rais kuwatumbua wakurugenzi wa Manispaa na Mabaraza kwa Unguja jambo ambalo liliwafurahisha wananchi kwa kua na kiongozi anaewajali na anaejitoa kusimamia maslah yao

 Licha ya Rais kua mkali kwenye hili lakini bado baadhi ya watendaji wamekua wazito katika kutekeleza hilo ambapo hali hyo imepeleea Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba kuuutaka Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo   kuweka uchambuzi kwa kuanisha kiwango cha fedha kilichotumika kwa kila mradi kulingana na kiwango cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya kutekelezwa miradi hiyo.

 Hayo yamejiri  baada ya kamati iliyoundwa kufanya uchunguzi wa mapato na matumizi halmashauri hiyo , ambapo  ripoti ya kamati hiyo imebainisha kwamba kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi hakuna fedha  yoyote iliyotumika kwa ajili ya kazi za maendeleo haliambayo inawavunja moyo wananchi ambao ndio walipa kodi

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Hamad Mbwana Shehe pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mohammed Mussa Mkobani wakawashauri madiwani hao kushirikiana kusimamia ukusanyaji wa mapato

 Mapema akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Ramadhan Nyerere Tosha amewataka madiwani kuendelea kuibua vyanzo vipya vya mapato ili kuongeza mapato ya Halmashauri.