Klabu ya Yanga rasmi imeingia Makubaliano ya Mkataba na Azam Media ya Mashirikiano ya Maudhui,mkataba ambao  wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 41 pamoja na VAT kwa Kipindi cha Miaka 10(sawa na bilioni 34.8 bila VAT)

Hafla ya Makubaliano hayo yamefanyika katika Hoteli ya Serena Jijin Dar Es Salam asubuh ya Tarehe 8 mwezi July Mwaka 2021 ambapo Azam Media waliwakilishwa na  Tido Mhando ambae ni Afisa mtendaji Mkuu wa Azam Media  na Klabu ya Yanga iliwakilishwa na Dr Mshindo Msolla ,ambae ni Mwenyekiti wa Klabu hiyo.

Mkataba huo wa miaka Kumi(10) itaiwezesha Klabu ya yanga katika Mwaka wa Kwanza kujikusanyia kila mwezi kutoka kwa Azam Media kiasi cha Shilingi Milioni Mia Mbilim za Kitanzania na Mwaka unaofuata itaongezeka Milioni Ishirini (20)

Mkataba huo pia umeipa nafasi yanga kujikusanyia bonas hadi shilingo Bilioni Tatu ikiwa kwa Kuanzia Msimu ujao Klabu hiyo Kongwe Barani Afrika itamaliza Msimu ikiwa katika nafasi mbili za Juu.

Klabu ya Yanga Afrika imetengeneza Rekodi  nyengine hii leo na kua klabu ya Kwanza Tanzania Kumiliki chaneli yake na Sio kipindi cha Dakika 30 kama ilivyo kwa Mahasimu wao Simba.

Ikumbukwe Yanga hivi Karibuni walifanya Mkatano Mkuu ambao sambamba na mambo mengine wanachama wa klabu hiyo walipitisha kwa Kauli Moja Ajenga ya Mabadiliko ya kikatiba ambayo itaiwezesha Yanga kuruhusu wawekezaji kwaajili ya Uwekezaji Mkubwa utakaoleta Faida kwa wanachama na Clabu kwa Ujumla

Mkataba huo unaweza kusema sasa Rasmi Yanga watakua wamewaacha mbali watani wao wa Jadi Simba kwakua bado Mkataba huo wa haki za maudhui haujawafikia.