Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Jamal Kassim Ali, amewateua wajumbe  wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais Fedha na Mipango imesema, kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 7(2), (c), (i), (ii), (iii) cha Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Namba. 2 ya mwaka 2005, amewateua wafutao kuwa wajumbe  wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF).

1. Bw.Arafat Ally Haji

2. Bw.Assaa Sharif  Khalid

3. Bw. Jaha Haji Khamis

4. Bi.Khadija Shamte Mzee

5. Bi. Sabra Omar Hussein

6. Bw.Said Abdalla  Basleym.

Uteuzi huo unaanza leo tarehe 20, July, 2021