Imeripotiwa kuwa watu wasiopungua 800 katika nchi ya Uganda iliyoko Afrika Mashariki walipewa chanjo ya bandia dhidi ya virusi vya corona (Kovid-19).

Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji wa Afya, Dk. Wallen Naamara, katika taarifa yake, alisema kuwa kesi za maambukizi ya Kovid-19 zinazoongezeka kila siku nchini zinatia wasiwasi.

Naamara alieleza,

"Watu wengine wasio waaminifu kwa nia ya kupata pesa nchini walidanganya umma katika zoezi la chanjo ya bandia ya Kovid-19."

Akibainisha kuwa angalau watu 800 walipewa chanjo ya bandia kati ya Mei na Juni nchini, Naamara alisema kuwa watu wengine walipewa maji badala ya chanjo.

Naamara pia alisema kuwa wauguzi wawili walizuiliwa katika uchunguzi uliozinduliwa juu ya tukio hilo, na daktari mhusika alikuwa akitoroka.

Akisisitiza kwamba chanjo ya Kovid-19 ni bure nchini, Naamara alitoa wito kwa umma kukaa mbali na chanjo hizo za kulipia.