ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewatahadharisha wananchi kujiepusha na ushiriki katika kampuni zinazojihusisha na ukusanyaji wa fedha taslim au njia ya mtandao kwa kigezo cha uwekezaji ili kuepusha upotevu wa mali zao.

 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango imeeleza kuwa shughuli hizo ambazo hufanywa na vikundi vya watu pamoja na baadhi ya Kampuni ikiwemo Kampuni ya Pama Funds, Qnet, Gameas, Wozur na nyenginezo sio salama.

 Pia Serikali imesisitiza mpango huo haupo chini ya usimamizi wa Serikali.

Tahadhari ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inakuja miezi kadhaa baada ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi kuingilia kati na kutaka kupatiwa ufumbuzi mgogoro wa Kampuni ya Masterlife Microfinance Ltd ambayo ilikusanya fedha kwa maelfu ya wananchi kinyume cha taratibu za nchi ambapo Rais Dkt. Mwinyi alitaka Kampuni hiyo kurudishia fedha kwa wananchi