wanajeshi sita wa Cameroon wameuwawa Jumamosi katika shambulio lililotekelezwa na Wanamgambo wa Boko Haram kaskazini kabisa mwa nchi hiyo.

Kupitia Runinga ya Serikali Gavana wa Mkoa huo amesema licha ya tukio hilo lakini wanajeshi wa Serikali bado wanaendelea kupambana.

Boko Haram walifanya shambulio kwenye kituo cha jeshi huko Sagme, karibu na mpaka na Nigeria, kaskazini kabisa mwa nchi hiyo Jumamosi asubuhi. Eneo ambalo Boko Haram imekuwa ikitekeleza mara kwa mara mashambulizi.

Idadi ya vifo ni angalau sita. Gavana wa mkoa wa kaskazini amewataka raia kushirikiana na vikosi vya ulinzi na usalama kwa kuwafichua wapiganaji na wanamgambo wa kundi la Boko Haram na waalifu wengine