Mwakilishi kutoka Taasisi ya Umoja wa Falme za Kiarabu Shekh Ahmed Al- Falasi ameahidi  kushirikiana na  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  kujenga Hospitali zitakazotoa huduma muhimu kwa jamii ili kuimarisha sekta ya afya nchini.

Ameyasema hayo wakati Akizungumza na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Mh Nassor Ahmed Mazrui  ofisini kwake Vuga Jijini Zanzibar.

Shehe Ahmed amesema taasisi hiyo imekusudia kujenga hospitali za kisasa Unguja na Pemba zitakazokua zikitoa huduma Muhimu sambamba na   kusaidia vifaa tiba katika hospitali kuu za Zanzibar .

Nae Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui  ameipongeza  Taasisi ya Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kuiunga mkono na kuisadia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye lengo la kuimarisha sekta ya afya nchini.

“Huduma  za afya zikiimarishwa kwa wananchi zitasaidia kuondoa usumbu uliopo na kutoa huduma nzuri kwa kijamii na kuleta kimaendeleo nchini”, alifahamisha Waziri Mazrui .

Waziri huyo alieleza kuwa pia taasisi hiyo inalengo la kuzisadia hospitali kuu za Unguja na Pemba kwa kuzipatia vifaa ili zipate kutoa huduma bora  kwa wananchi na kuondosha usumbufu uliopo nchini .