Karibu wiki ya Pili sasa bado maeneo mbali mbali ya
Tanzania Mjadala Mkubwa unaojadiliwa ni kuhusiana na Sheria Mpya ya Tozo katika
simu.
Viongozi mbali mbali wamekua wakitolea ufafanuzi
hilo lakini hata Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasan
alilizungumzia na kuitaka wizara kutafakari malalamiko ya wananchi
Sheia hii kama ilivyo kawaida imejadiliwa na
kupitishwa na Bunge,hivyo wengi wakatamani kujua Spika wa Bunge la Jamhuri wa
Muungano wa Tanzania Job Ndugai anasemaje katika hili
Kufuatia hilo Spika Ndugai kwaupande wake amepigilia
msumari kwenye tozo ya miamala katika simu kwa kudai Bunge ndio limepitisha na
wale ambao wanapinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala nini kifanyike.
Amesema Lengo la Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania ifikapo Mwaka 2025 Tanzania Iwe Nchi ya Mfano katika suala la
Maendeleo ikiwemo Miundombinu ya Barabara,Afya na Maji
Akizungumza
leo, Julai 23, 2021, katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa
Dodoma, Anthony Mtaka, amesema wao kama Bunge ndio wameamua kuwe na tozo katika
miamala ya simu kwa sababu fedha zitakakazopatikana zitaenda katika mfuko
Maalum ambao utawasaidia wananchi.
"Tumepitisha sisi, tukatunga sheria sisi,
tunataka kuliona hilo, sasa wewe ambaye unapinga tupe njia mbadala tutapata
wapi fedha, tunafikaje 2025, kwa hiyo maamuzi ni hayo tumeyafanya, kwa nia
njema kabisa kwamba 2025 tuwe tumetoka, tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni
tofauti... CCM hoyee, nimemaliza
Spika Ndugai ameyazungumza hayo kufuatia baadhi ya
wananchi kulalamika kwamba kumekuwa na tozo kubwa katika miamala ya simu.





0 Maoni