Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira kilichotokea leo tarehe 22 Julai, 2021 katika hospitali ya Rufaa ya Mount Meru mkoani Arusha alipokuwa akipatiwa matibabu.

 Mhe. Rais Samia amesema amepokea taarifa za kifo cha Mhe. Anna Mghwira kwa majonzi na masikitiko makubwa hasa akikumbuka mchango wake mkubwa alioutoa katika ujenzi wa taifa.

 Amewaomba wanafamilia wote wawe na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amemuombea marehemu Anna Mghwira apumzike mahali pema peponi, Amina.

Anna Mgwira aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, na mgombea urais kupitia chama cha ACT-Wazalendo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015

 Mama Anna Elisha Mghwira, amefariki dunia leo wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru, Arusha.

Imeelezwa kuwa Mama Mghwira amefariki dunia leo Julai 22, 2021, majira ya mchana, ambapo taarifa zinadai kwamba wiki moja iliyopita alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Nkoaranga kwa tatizo la kupumua ambapo baadaye hali yake kuwa mbaya alihamishiwa hospitali ya Mount Meru hadi  umauti ulipomkuta.


Mh Anna Mgwira aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mwenyekiti wa Chama cha Act