MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Kaskazini Pemba, Asiya Sharif Omar, ameitaka jamii kutambua kuwa watoto wenye ulemavu bado wanahitaji kuthaminiwa pamoja na kupatiwa misaada yote kama wanavyopatiwa watoto wasio na ulemavu nchini.
Amesema ulemavu wao isiwe ni chanzo cha kukosa
thamani kwa jamii, pamoja na kutokupatiwa haki zao stahiki ikiwemo suala zima
la elimu, afya na huduma muhimu za kijamii.
Mbunge Asiya ameyasema hayo wakati wa hafla ya
kukabidhi misada mbali mbali kwa watoto wenye ulemavu, ikiwemo baskeli, taulo
za kike, mchele na fedha taslimu huko Ungi Msuka Wilaya ya Micheweni.
Amesema utoaji wa msada huo ni utekelezaji wa
ulani ya CCM, kwani CCM haina ubaguzi katika suala zima la kuwapatia wananchi
wake maendeleo.
Naye mwakilishi wa jimbo la Konde Zawadi Amour
Nassor, amesema msaada huo umekuja kwa wakati muwafaka, kwani watoto hao
wamekuwa pata tabu wanapohitaji kutembea.
Aidha amepongeza uongozi wa UWT kwa juhudi
zake mbali mbali wanazozichukua katika kuhakikisha wanawake wanafaidika kupitia
miradi wanayoianzisha katika maeneo yao.
Nao wazazi wa watoto hao, wamemshukuru mbunge
huyo kwa kutekeleza ahadi zake kwa vitendo na kuwasaidia watoto hao kuwapatia
vibaskeli, ambavyo vitawasaida katika kutembea.
ANGALIA TUKIO ZIMA HAPA CHINI





0 Maoni