Ikiwa kesho Waislam Duniani kote wanaungana  katika kusheherekea sikukuu kubwa ya Kidini ya Eid El Haj viongozi mbali mbali kupitia mitandao ya kijamii wameonekana wakirusha Jumbe mbali mbali za kuwatakia Kheri na fanaka wananchi wao katika siku hiyo Muhimu.

Kupitia mitandao ya kijamii Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Asia Sharif Omar amewatakia Kheri ya Sikukuu Waislam wote na Watanzania kwa ujumla.

Katika Ujumbe wake wapili amewataka wazazi kuhakikisha wanakua wakini na watoto wao hasa wanapokwenda katika kumbi za skukuu ili kuwaepusha Watoto kutofanyiwa vitendo vya udhalilishaji

"Naendelea kuwahimiza wakinamama katika kusheherekea skukuu hii wahakikishe wanakua makini na Watoto wao wanapokwenda kwenye maeneo ya skukuu ili kumuepusha mtoto asifanyiwe vitendo vya udhalilishaji. Tunaamini Zanzibar bila ya udhalilishaji inawezekan"

Skukuu ya Eid El Haj au Eid al-Adha maana yake ni "sikukuu ya kutoa kafara/kuchinja" kwa Kiarabu na hutumiwa kukumbuka wakati nabii Ibrahimu alipotaka kumtoa kafara mwanawe Ishmael alivyoamriwa na Allah, lakini akapewa kondoo na Mungu amtoe kafara badala yake.

 

Sikukuu ya Eid ul-Adha huadhimishwa kuanzia siku ya 10 tangu kuonekana kwa mwezi wa Dhul Hijjah.