Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kasakazini Pemba Mh Asiya Sharif Omari ametuma salam za Rambirambi kwa ndugu jamaa na  Marafiki kufuatia Msiba wa aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Anna Mgwira

Katika salam zake hizo Mhe.Asiya amemzungumzia Marehemu Anna Mgwira kuwa alikua mwanamke Mpambanaji na aliekuwa akijitoa katika kipindi chake chote cha uongozi alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

Amesema Taifa limepoteza Mtu Muhimu ambae alikuwa Mzalendo wa Taifa lake na Mpenda maendeleo aliekua akisimama katika kutatua Changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi

‘’kiukweli Anna Mgwira licha ya  kuwa nimemfahamu mda mrefu lakini pia alikua mwanachama mwenzangu wa Chama cha Mapinduzi,kwahyo nasema nimpambanaji na aliekuwa akijituma katika majukumu yake na tumeshuhudia kipindi cha Uongozi wake Mkoa wa Kilimanjaro alikua akishuhulika sana na kutatua changamoto za Wananchi bila kumbagua mtu kwa itikadi ya chama ama Dini’’alisema Mhe.Asiya Sharif

Anna Elisha Mghwira, amefariki dunia leo wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru Arusha

Imeelezwa kuwa Mama Mghwira amefariki dunia leo Julai 22, 2021, majira ya mchana, ambapo taarifa zinadai kwamba wiki moja iliyopita alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Nkoaranga kwa tatizo la kupumua ambapo baadaye hali yake kuwa mbaya alihamishiwa hospitali ya Mount Meru hadi  umauti ulipomkuta.