Uongozi wa klabu ya Yanga Sc umethibitisha kuwa tayari wamewasilisha ushahidi wa kesi dhidi ya mchezaji Bernard Morrison na kinachosubiriwa sasa ni kutolewa hukumu kwa kesi hiyo

Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa Michezo (CAS) inatarajiwa kutoa hukumu ya kesi hiyo kabla ya mwezi huu kumalizika

Uamuzi wa Kesi hiyo Inaelezwa itatolewa maamuzi na CAS Julai 22 na Jaji kutoka nchini Uingereza

Mapema wiki hii katika mahojiano katika kituo kimoja cha Tv Jijini Dar Es Salam, Afisa Habari wa Yanga Sc Hassan Bumbuli alizungumza kuwa Yanga Sc itakuwa bingwa msimu huu na jambo hilo litatokea kabla ya Julai 25 siku ya mchezo wa fainali kombe la FA

"Tuna michezo miwili kukamilisha msimu, Julai 14 tutacheza na Ihefu Fc na Julai 18 Dodoma Jiji, tunahitaji kushinda mechi zote mbili. Naamini tutakuwa mabingwa msimu huu, tena jambo hilo litatimia kabla ya mchezo wa fainali ya FA," alitamba Bumbuli