Mkuu wa wilaya ya magaharib  A Suzan Peter Kunambi  ameutaka  uongozi wa shule ya mbuzini na kamati ya skuli hiyo kuondosha tofauti zao ambazo zinazopelekea migogoro ya chini kwa chini ili kuepusha  kurudisha nyuma  maendeleo ya elimu katika skuli hiyo.

 Akitoa kauli hiyo wakati akisikiliza  changamoto za skuli katika kikao cha pamoja kati ya wazazi  kamati ya skuli na walimu kilichofanyika skuli ya mbuzini.

Amesema  kuendelea kwa mgogoro hiyo hasa wakati huu ambapo wanafunzi wanajiandaa na mitihani ya Moko na Mitihani ya Taifa si jambo jema kwani kutazorotesha maendeleo ya skuli hiyo na kupunguza kiwango cha  upasishaji kwa wanafunzi.

 Nao wazazi waliohudhuria Kikao hicho wamesema watalitekeleza kwa vitendo agizo la Mkuu wa Wilaya kuondosha Migogoro katika Shule hiyo  ili kuongeza ufaulu kwa watoto wao.