Makamo wa Pili wa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh Hemed Suleiman Abdullah akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Konde katika Mkutano wa kufunga kampeni za Kumnadi Mgombean Ubunge wa Ccm katika uchaguzi Mdogo Jimboni hapo.
Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Konde Mh Sheha Mpemba Faki akionyesha Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa Wananchi wa Konde waliojitokeza katika ufungaji wa shuhuli za Kampeni katika Viwanja vya Konde mjini.

      Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Asia Sharif Hamadi(kulia) akizungumza jambo na Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Konde Mh Sheha Mpemba Faki

Na Suleiman Mohamed, Pemba

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamia kutengeneza kwa kiwango cha Lami barabara zote za unguja na Pemba ili kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili wananchi kutokana na uchakavu wa baadhi ya barabara kubwa na zile za ndani.

Hayo yameelezwa  hapo Jana na Makamo wa Pili wa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibara Mh Hemed Suleiman Abdullah katika Viwanja vya Konde Mjini ,Mkoa wa Kasakazi Pemba, wakati akifunga kampeni za kumnadi mgombea nafasi ya ubunge wa Chama cha mapinduzi .

Amesema tayari Serikali imejianda karibuni kuwaleta wakandarasi katika maeneo yote ya Barabara yaliyoainishwa Unguja na Pemba kwaajili ya kuanza ujenzi ambapo Kilometa Zaidi ya Mia nne na Ishirini zikiwemo Barabara Kuu na zile za Ndani zinataraajiwa kujengwa kwa kiwango cha Lami.

Amezitaja baadhi ya barabara zitakazonufaika kwa upande Jimbo la Konde  ni Konde- Msuka,Konde Makangale,Konde-Kipange na Konde- Ungi ,ambapo amesema ujenzi huo utaanza na kukamilika kwa muda mfupi kutokana na barabara nyingi kilometa zake kutokuwa na ubali mrefu.

Katika hatua nyengine Mh  Hemed amewataka wananchi wa Jimbo la Konde kumchagua Mgombea wa nafasi ya Ubunge atokanae na Chama cha Mapinduzi (CCM) ndugu Sheha Mpemba Faki ili akasimamie yale ambayo Serikali ya Ccm imedhamiria kuyafanya katika Jimbo hilo

Amesema kufanya hivyo wataweza kulifanya Jimbo la Konde kupiga hatua za kimaendeleo kwakua Mgombea huyo atokanae na Chama cha Mapinduzi nimchapa kazi na anajua shida za wananchi wa Konde.

Uchaguzi  Mdogo kuziba nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Konde unatarajiwa kufanyika kesho tarehe 18-07-2020 ambapo uchaguzi huo unfanyika kufuatia kufariki Dunia kwa aliyekua Mbunge wa Jimbo hilo Mh Khatib Said Haji Alhamis ya Mei 20.

Naibu katibu Mkuu Zanzibar Dr Abdallah Sadala Mabodi(kulia) akimtunza Pesa Mh Mwakilishi wa Jimbo la Konde Zawadi Amor(kushoto) baada ya kuzungumza jambo lililofurahisha wanachi waliokuwa wanafuatilia Mkutano huo
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Asia Sharif Hamadi(kulia) akizungumza jambo na Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Konde Mh Sheha Mpemba Faki

wabunge na wawakilishi wa Kisiwan Pemba watokanao na Chama cha Mapinduzi wakifurahia jambo katika shuhuli za kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la  Konde  Mh Sheha Mpemba Faki